WATU 11 wakiwemo watoto watatu hawajulikani waliko baada ya Jahazi walilokuwa wakisafiria kutoka Tanga kwenda Zanzibar kupata dhoruba na kuzama karibu na visiwa vya Zanzibar majira ya saa 11 za alfajiri leo.
Akizungumza kutoka Hospitali ya Kaskazini A Kivunge nahodha wa Jahazi hilo Abdullah Saleh, ambaye amenusurika alisema jahazi hilo lilikuwa limepakia abiria 32, lakini lina uwezo wa kupakia abiria 50.
Alifafanua kuwa safari yao ilianzia Tanga majira ya Saa nane za Usiku lakini hali ya hewa ilibadilika ghafla majira ya saa 11 alfajiri na kusababisha Chombo hicho kuzama.
Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati ya maafa Zanzibar amewapa pole abiria waliokolewa baada ya kuwatembelea hospitalini hapo ambapo pia alimpongeza nahodha wa chombo hicho kutokana na kushiriki kikamilifu kwenye zoezi la kuokoa abiria waliozama kwenye chombo hicho.
Akizungumza kutoka Hospitali ya Kaskazini A Kivunge nahodha wa Jahazi hilo Abdullah Saleh, ambaye amenusurika alisema jahazi hilo lilikuwa limepakia abiria 32, lakini lina uwezo wa kupakia abiria 50.
Alifafanua kuwa safari yao ilianzia Tanga majira ya Saa nane za Usiku lakini hali ya hewa ilibadilika ghafla majira ya saa 11 alfajiri na kusababisha Chombo hicho kuzama.
Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati ya maafa Zanzibar amewapa pole abiria waliokolewa baada ya kuwatembelea hospitalini hapo ambapo pia alimpongeza nahodha wa chombo hicho kutokana na kushiriki kikamilifu kwenye zoezi la kuokoa abiria waliozama kwenye chombo hicho.
No comments:
Post a Comment