MATUNDA YA GESI YAANZA KUPATIKANA WILAYANI KILWA. - RAHA ZA PWANI

Habari za Hivi Punde

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Friday, February 1, 2013

MATUNDA YA GESI YAANZA KUPATIKANA WILAYANI KILWA.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kilwa, Addo Mapunda (aliyekaa kushoto)akitiliana saini na  Bi Anne Devilliers, Mratibu wa Mradi wa mpango wa ufundishwaji wa Lugha ya Kingereza kwa njia ya teknolojia ya kisasa (Techonologe Enhanced Edcation) TEE-TZ chini ya ufadhili wa kampuni ya Pan African Energy, inayojishughulisha na kazi ya uchimbaji, usambazaji na uuzaji wa gesi asilia ya Songosongo
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa Addo Mapunda (kushoto) akibadilishana mkataba na mratibu wa mpango huo Bi Anne Devilliers. Mpango huo utazinufaisha shule mbalimbali za sekondari wilayani humo.  
WANAFUNZI wapatao 1580 wa shule tisa za sekondari Wilayani Kilwa Mkoani Lindi wanatarajiwa kunufaika na mpango wa elimu wa mafunzo ya lugha ya Kingereza kwa njia ya Technolojia ya kisasa TEE-TZ chini ya ufadhili wa kampuni inayojihusisha na uchimbaji, usambazaji na uuzaji wa gesi asilia ya Songosongo.
Mradi huo wa miaka mitatu unatarajiwa kugharimu kiasi cha Tsh.144,945,218. Zitakazotumika kujenga misingi bora ya lugha ya kingereza kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza kuanzia mwaka 2013.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Adoh Mapunda wakati akitoa taarifa kwenye hafla fupi ya utiaji saini wa mpango huo.
 Mafunzo hayo yaliyoanza hivi karibuni yanatolewa na walimu wapatao 30, wakiwemo wakigeni 12(Volunteeers) na wazawa 18, ambapo kwakuanzia yanatarajiwa kufanyika kwa wiki 6.

Kwenye Shule hizo tisa kila moja italazimika kutoa walimu wawili ambao watapatiwa mafunzo kwaajili ya kuendeleza mpango huo katika shule zote.

Mkurugenzi huyo alizitaja shule zitakazonufaika na mpango huo ni, Kilwa day iliyopo mji mdogo wa Kilwa masoko, Mtanga, Songosongo, Mbuyuni,Kinjumbi, Miteja, Mingumbi, Kikanda na Sekondari ya wasichana Ilulu.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here