Hans Pope ambeba Alphonce Modest - RAHA ZA PWANI

Habari za Hivi Punde

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Thursday, September 6, 2012

Hans Pope ambeba Alphonce Modest

Mkurugenzi wa Msama Promotions, Alex Msama (kushoto) akimkabidhi msaada wa fedha taslimu sh. milioni moja mchezaji wa zamani wa Simba, Mtibwa na Taifa Stars, Alphonce Modest kwa ajili ya kumsaidia katika matibabu ya ugonjwa wa mifupa unaosababisha miguu kufa ganzi ‘yabisi baridi’. Modest nasumbuliwa na ugonjwa huo tangu mwaka 2011. Kwa yeyote anayeguswa na tatizo lake awasiliane na mtangazaji wa Chanel 10, Said Kilumanga (wa pili kulia) kwa kupitia namba 0718 427426. Wa Pili kushoto ni Mhariri Kiongozi wa Champion, Saleh Ally.


Na Mwandishi Wetu
 
MWENYEKITI wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zakaria Hans Pop ametoa msaada wa dola 1000 (zaidi ya Sh milioni 1.5) kwa beki wa zamani wa timu hiyo, Alphonce Modest anayesumbuliwa na maradhi ya ganzi.
Zacharia Hans Poppe.
 
 
Modest yuko jijini Dar es Salaam akiendelea na matatibu chini ya usimamizi wa gazeti la Championi kwa kushirikiana na kipindi cha michezo cha radio ya Magic FM.
 
Akizungumza na Championi Ijumaa,    Mtangazaji wa Magic FM, Said Kilumanga ambaye ni mmoja wa waratibu wa zoezi hilo alisema tayari Hans Pop ameshakabidhi fedha hizo.
 
 “Tunamshukuru sana Hans Pop kwa moyo wa kujitolea, wengine pia wajitokeze kumsaidia kwa kuwa amepungukiwa kama Sh 600,000 tu ili kukamilisha matibabu yake,” alisema Kilumanga.
 
Mkurugenzi wa Msama Promotion, Alex Msama ndiye alikuwa mdau wa kwanza kumchangia Modest na kuomba wengine wajitokeze kumsaidia beki huyo mahiri wa zamani.
 
Baadhi ya wanamichezo wamekuwa wakiendelea kumchangia Modest ili kuhakikisha anapata matibabu baada ya maradhi hayo kumuandama kwa zaidi ya miaka minne sasa.
 
Kwa wengine walio tayari kumsaidia, wanaweza kuwasiliana au kutuma michango yao kupitia namba zifuatazo 0718427426 narudia tena 0718427426.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here