Shule ya kanisa yashambuliwa Nairobi - RAHA ZA PWANI

Habari za Hivi Punde

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Sunday, September 30, 2012

Shule ya kanisa yashambuliwa Nairobi

Polisi Jijini Nairobi wakipekua mabaki ya vifaa vya shule vilivyolipuliwa na guruneti leo asubuhi ambapo mwanafunzi mmoja aliuwawa kwenye shule ya Saint Polycarp.
-->
Askari wa Kenya wakiangalia eneo ambalo guruneti lillipita kwenye shule hiyo.

Shambulio la guruneti la mkononi dhidi ya shule ya Jumapili ya watoto wa Kikristo mjini Nairobi limeuwa mtoto mmoja na kujeruhi wengine kadha.
Mkuu wa polisi wa Nairobi, Moses Ombati, ameliambia gazeti la Daily Nation kwamba watu watatu wamekamatwa, na kwamba watu hao walionekana wakipiga picha za kanisa la Saint Polycarp lilolengwa.
Msikiti ulio karibu na hapo ulishambuliwa na vijana waliokuwa na hasira.Afisa wa polisi wa Nairobi aliwasihi watu wawe watulivu. Shambulio lilitokea katika mtaa wa Juja Road, unaopakana na mtaa wa Eastleaigh.
Inaaminiwa kuwa guruneti lilirushiwa kanisa la Saint Polycap kama saa tano punde baada ya misa ya asubuhi.
Wakati huohuo
Kundi lilokuwa na hasira limewashambulia Wasomali katika mtaa wa Eastleigh, Nairobi, baada ya guruneti kurushwa kwenye shule ya Jumapili ya watoto wa Kikristo, na kuuwa mtoto mmoja na kuwajeruhi kadha.
Polisi wakilinda mtaa wa Nairobi
Polisi waliwatawanya vijana ambao waliwalenga Wasomali wa mtaa wa Eastleigh. Polisi wanasema watu 13 walijeruhiwa katika mashambulio hayo ya kulipiza kisasi. Katika mashambulio ya karibuni dhidi ya makanisa nchini Kenya, wamelaumiwa wapiganaji wa Kiislamu, al-Shabaab wa Somalia, ambako wanajeshi wa Kenya wakishirikiana na wale wa Umoja wa Afrika wanapambana na wapiganaji hao.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here