TMF Yawanoa Wanahabari na Wamiliki wa Vyombo vya Habari Mkoani Lindi - RAHA ZA PWANI

Habari za Hivi Punde

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Monday, October 8, 2012

TMF Yawanoa Wanahabari na Wamiliki wa Vyombo vya Habari Mkoani Lindi

Mshauri wa mambo ya Habari ambae pia ni mwandishi Mkongwe,Bw Ndimara Tegambwage akitoa mafunzo kwa waandishi na wamiliki wa vyombo vya habari mkoani humo leo.
Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania katika kukuza Uimara Na kujenga Uhuru wa Vyombo vya habari na Waandishi wa Habari unatoa mafunzo kwa kwa Waandishi na wamiliki wa vyombo hivyo Mkoani Lindi ili kuwajengea
Uwezo wa kuomba Ruzuku zinazotolewa na Mfuko huo

Mafunzo hayo ya Siku moja yanawezeshwa na Mshauri wa mambo ya Habari ambae pia ni mwandishi Mkongwe,Bw Ndimara Tegambwage na Meneja wa Vyombo vya Habari vya SJMC Chini ya Chuo kikuu cha DSM,Bi Edda Sanga
Kufuatia awamu ya pili ya Utoaji Ruzuku hizo toka TMF,Mfuko umeamua kutoa mafunzo hayo ili kutoa msisitizo katika Uandishi wa Habari za Vijijini,Uwazi na Uwajibikaji,Utawala bora,Ukimwi,Jinsia na kuwapa sauti za jamii zilizotengwa ili waandishi waweze kupata habari kwa jamii na habari zinazogusa jamii

Katika Mafunzo hayo pamoja na kuwezesha na wakongwe wa habari pia yamehusisha wanahabari na wamiliki toka mkoani humo yanayoweshwa na Afisa Mwandamizi wa TMF,Alex Kanyambo,Afisa Mawasiliano TMF,Japhet Sanga na Bi Raziah Mawanga,,,Afisa Mafunzo Tmf . Picha na Habari..Mdau Abdulaziz video,Lindi

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here