GREDA LAGONGA MWENDESHA BODABODA NA ABIRIA WAKE MJINI MUSOMA JIONI HII. - RAHA ZA PWANI

Habari za Hivi Punde

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Friday, December 21, 2012

GREDA LAGONGA MWENDESHA BODABODA NA ABIRIA WAKE MJINI MUSOMA JIONI HII.

Mwanamke ambaye jinalake halikuweza kufahamika maramoja akiwa amelala chini baada ya bodaboda aliyokuwa amepanda kugongwa na greda lakuchonga barabara kwenye ajali mbaya iliyohusisha Greda na Bodaboda. Ajali hiyo imetokea alasiri hii mjini Musoma kwenye makutano ya Barabara ya Shabani na Bus Stop. Ajali hiyo imepelekea abiria aliyekuwa amepakiwa katika pikipiki hiyo kujeruhiwa vibaya maeneo ya tumbo baada ya kuburutwa na mashine hiyo ya kutengenezea barabara. Hata hivyo limetokea gari la shirika la umeme Tanesco na kumchukua majeruhi huyo na kumkimbiza katika hospitali ya Mkoa wa Mara. Mpaka mwandishi wetu anaondoka eneo la tuio kulikuwa na sintofahamu ya ni wapi dereva wa pikipiki na greda hilo walipoelekea kwani mashuhuda wa tukio hilo wanasema dereva wa pikipiki alikimbia punde tu ajali ilipotokea.

Pikipiki iliyohusika kwenye ajali hiyo!
Wananchi waliofika kushuhudia tukio hilo! Picha kwa hisani ya Mara yetu.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here