AMCHOMA MWANAWE MOTO KWA WIZI WA BOGA. - RAHA ZA PWANI

Habari za Hivi Punde

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Thursday, May 31, 2012

AMCHOMA MWANAWE MOTO KWA WIZI WA BOGA.


 Na Ahmed Abdullaziz Lindi.
 KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida mama mmoja Sabina Silvestre, mkazi wa kijiji cha Mtandi, wilaya ya Kilwa Mkoani LINDI, amemchoma moto mikono yote miwili mwanaye wa kumzaa mwenye umri wa miaka minne kwa madai ya kuiba boga.
Mama huyo amedai kuwa baada ya kubaini mwanaye amechukua boga bila kuomba akamchukua na kumfunga  kamba mikononi pamoja  na majani makavu kisha akachukua kibiriti na kuuwasha moto katika mikono ya mwanaye na kuuanza kumuunguza.
Mtoto huyu mwenye umri wa miaka minne anayejulikana kwa jina la Noel John, amechomwa moto mikono yake miwili na mama yake mazazi kwa madai ya kuiba boga, na kisha kumficha ndani kwa siku tano bila kumpeleka hospitali ,ndipo wasamaria wema wakatoa taarifa kwa Afisa Mtendaji Kijiji cha MTANDI Makarani Mjaka.
"Ni kweli ndugu mheshimiwa mama huyo amemchoma moto mwanaye kwa kumfunga na majani makavu mimi nilipata taarifa kutoka kwa raia wema nilipofika nyumbani kwake ni kweli nikamkuta mama huyo akiwa na mwanaye, nikamuhoji akakubali kuwa amefanya hivyo, mimi kama mtendaji nikamchukua hadi ofisini kwa mahojiano zaidi na baada ya hapo nikampeleka katika mahakama ya hapo kijijini kwa taratibu zingine , kwa upande wangu nilifanya hivyo kama mtendaji, pia mtoto nilimpeleka hospitalini kwa matibabu na ameanza kupata tiba na kuandikiwa sindano tano na gharama ni yangu mimi mtendaji wa kijiji cha Mtandi.
 Mama mzazi wa mtoto huyu Sabina Silvester,alieleza kilichomsibu Alichukua boga kwa shemeji yangu na kulileta nyumbani, akanambia mama shemeji kakupa boga upike, mara shemeji yake akatokea na kuchukua boga, mama huyo akamuuliza mwanaye mbona ulichukua boga bila kuomba mtoto akanyamaza kimya, mara pili tena kamuuliza mtoto kanyamaza kimya ndipo mama huyo akamkamata mwanaye akachukua majani makavu na kamba akamfunga mikononi kisha akachukua kibiriti akawasha na moto ukawaka mtoto ndio hivyo akaanza kuungua.Sijampeleka hospitali nilikuwa nampa mitishamba tu kwa sababu hela sikuwa nayo.
Bila woga akasema Mimi naomba nawaomba akina mama wenzangu wenye roho mbaya kama mimi wasifanye hivyo kama mimi, waache, mimi najiuliza ni kwa nini lifanya hivyo kwa mwanangu
JOHN RAFAEL Baba mazazi wa mtoto huyu anadai wakati tukio linatokea  hakuwepo lakini mmh Mimi nilikuwa shambani niliporudi nikamkuta mtoto yuko hivyo, nikamuuliza mke wangu kwa nini umefanya hivyo akanijibu kwamba mtoto huyu si wako, sasa mimi baada ya mke wangu kunijibu hivyo kikapata hasira nikaondoka zangu, kurudi nakuta mtendaji amempeleka mtoto hospitali namshukuru sana.
Kwa upande wao majirani wanaoishi karibu na mama huyo wamesikitishwa na kitendo hicho na kuomba sheria ichukue mkondo wake dhidi ya wanawake wanaofanya ukatili kwa watoto
Mwajuma Said- Mama huyu achukuliwe hatua kabisa haiwezekani mtoto kwanza alimpiga sana kaona haitoshi kamchoma moto anatuzalilisha akina mama wenzake hapa kijijini, hana huruma ni mkatili sana yaani alidiriki kuchukua majani makavu na kumfunga nayo mtoto na kumuwashia kibiriti.
Rashid Sufiani- Jamii isiwachukie watoto na kuwafanyia vibaya kama mama huyo, watoto pia wana haki kama ilivyo kwa watu wazima wasiwapige, akina mama acheni ukatili.
Asha Juma- Mimi kama mtoto naomba akina mama wasituchome moto
Pia mwendesha mashitaka huyo alidai kwamba kutokana na kitendo hicho,mshitakiwa amemsababishia mlalamikaji maumivu  makali kwenye mwili wake. 
Aidha,Mwahija aliiambia mahakama hiyo kwamba kutokana na kitendo hicho mshitakiwa amefanya kosa chini ya kifungu cha 225 kanuni ya adhabu sura ya 16. 

Mshitakiwa amekana kosa linalomkabiri na amepelekwa rumande,baada ya upande wa mashitaka kupinga dhamana kwa mshitakiwa kutokana na kutopata taarifa ya maendeleo ya mlalamikaji,kesi hiyo namba 49/2012,itatajwa tena Juni 11 mwaka huu.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here