UKATILI DHIDI YA WANAWAKE WAENDELEA NCHINI. - RAHA ZA PWANI

Habari za Hivi Punde

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Thursday, May 31, 2012

UKATILI DHIDI YA WANAWAKE WAENDELEA NCHINI.



Na Ahmed Abdullaziz Lindi.

MTU Mmoja amefikishwa mahakama ya wilaya ya Lindi akikabiliwa na Shitaka moja la kumjeruhi kwa kumchoma na moto wa pasi mke wake.

Mwanzaga Degratius Mbowi (44), amefikishwa mahakamani hapo na kusomewa Shitaka lake na mwanasheria wa Serikali, Mwahija Ahamadi. 

Akimsomea Shitaka lake mbele ya Hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama hiyo, Dustan Ndunguru, mwendesha mashiataka huyo akadai kuwa mei 27 mwaka huu, saa 1:30 asubuhi,huko mtaa wa Wailes katika Manispaa ya Lindi,mshitakiwa alimjeruhi kwa kumchoma moto mke wake wa ndoa Olifoncia Chembe. 

Mwahija aliiambia mahakama hiyo kwamba siku na wakati huo mshitakiwa na mke wake huyo wote kwa pamoja walikuwepo nyumbani kwao na mara kukatokea kidogo mifarakano ambayo yalimpelekea mshitakiwa kumpiga na hatimaye kuchukua pasi ya moto na kumuunguza mlalamikaji mkono wake wa kulia na sehemu nyingine. 

Pia mwendesha mashitaka huyo alidai kwamba kutokana na kitendo hicho,mshitakiwa amemsababishia mlalamikaji maumivu  makali kwenye mwili wake. 

Aidha, Mwahija aliiambia mahakama hiyo kwamba kutokana na kitendo hicho mshitakiwa amefanya kosa chini ya kifungu cha 225 kanuni ya adhabu sura ya 16. 

Mshitakiwa amekana kosa linalomkabili na amepelekwa rumande,baada ya upande wa mashitaka kupinga dhamana kwa mshitakiwa kutokana na kutopata taarifa ya maendeleo ya mlalamikaji, kesi hiyo namba 49/2012, itatajwa tena Juni 11 mwaka huu.

Mwisho.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here