BREAKING NEWS RAIS WA MAURITANIA APIGWA RISASI. - RAHA ZA PWANI

Habari za Hivi Punde

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Sunday, October 14, 2012

BREAKING NEWS RAIS WA MAURITANIA APIGWA RISASI.

Rais wa Mauritania, Mohamed Ould Abdel Aziz pichani, anapelekwa Ufaransa kwa matibabu zaidi baada ya kujeruhiwa alipopigwa risasi.
Kabla ya kuondoka kuelekea Paris, Rais Abdel Aziz alisema kwenye hotuba iliyotangazwa kwenye televisheni kutoka hospitali, kwamba ameshafanyiwa upasuaji ambao ulifanikiwa.
Wakuu walisema rais alijeruhiwa wakati wanajeshi wa serikali waliokuwa kwenye doria, walipofyatulia risasi msafara wa rais. Inaarifiwa kuwa maafisa wawili wa jeshi wamekamatwa.
Jenerali Abdel Aziz, ambaye anaonekana na mataifa ya magharibi kuwa anasimama dhidi ya wapiganaji wa Kiislamu katika eneo hilo, alichaguliwa mwaka wa 2009, mwaka mmoja baada ya kupindua serikali.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here