|
Daktari wa Macho akimfanyia uchunguzi mgojwa wa macho Upendo
Kisese huku Mkuu wa Mkoa akishuhudia kwenye viwanja vya Biafra jijini Dar es
Salaam leo wakati wa maadhimisho ya siku ya macho duniani.
|
|
Msimamizi wa Kitengo Cha macho Manispaa ya Ilala Ramadhani
Msuya, akimpima mgonjwa wa macho Ustadh
Abuu Yusuph wakati wa Maadhimishohayo ambapo huduma hizo zinatolewa bure kwa
siku nzima.
|
TAKWIMU:
KULINGANA na takwimu za Shirika la Afya
Duniani, inakadiriwa kuwa zaidi ya watu milioni arobaini na tano (45,000,000)
hawaoni na watu milioni mia mbili sitini na tisa (269,000,000) wana uoni hafifu
duniani kote. Asilimia 4 ya wakazi wa dunia hii wana uoni hafifu/upofu. Asilimia
90 ya watu wenye upofu ni wakazi wa nchi zinazoendelea.
Jambo
la kutia moyo ni kwamba wataalam wamethibitisha ya kwamba asilimia 80 ya
matatizo hayo yanayosababisha kutokuona yanazuilika au kutibika.
Hapa
kwetu Tanzania inakadiriwa kuwa ni zaidi ya watu 400,000 ambao ni sawa na
asilimia 1 ya wakazi wa nchi nzima. Asilimia 3 ya watanzania (takribani watu
zaidi ya milioni 1.2) wana uoni hafifu na kila mwaka watanzania zaidi ya 70,000
wanakuwa vipofu kutokana na sababu mbalimbali.
Upofu huu husababishwa kwa kiwango kikubwa
na magonjwa au hali zifuatazo:-
1).
Cataract (mtoto wa jicho) 50%
2).
Ukungu wa kioo cha jicho (cornea) 20% - ambao
husababishwa na trachoma au upungufu wa Vitamin A
3).
Glaucoma (presha ya macho) 10%
4.
Matatizo mengine - 20%. (Kisukari, magonjwa ya Retina
refractive errors na low vision).
Hali ya huduma za macho Mkoa wa Dar es
Salaam:
Historia
fupi ya huduma za macho katika Mkoa wa Dar es Salaam.
Huduma
ya macho ilianzishwa mwaka1970 - Hospitali ya Muhimbili. Mwaka1978 ilianzishwa
kwenye Zahanati ya Mnazi mmoja. Baada ya hapo huduma zilianza kutolewa Manispaa
ya Temeke na Kinondoni mwaka 1990, hatimaye mwaka 1994 zilianzishwa CCBRT.
Mkoa
wa DSM una vituo vya huduma ya macho vya serikali 9, binafsi 6, na vituo
vingine vya kutoa huduma ya miwani.

No comments:
Post a Comment