JAJI LUBUVA ATAKA Z'BAR IWE DOLA NA TANGANYIKA IWE DOLA. - RAHA ZA PWANI

Habari za Hivi Punde

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Thursday, January 24, 2013

JAJI LUBUVA ATAKA Z'BAR IWE DOLA NA TANGANYIKA IWE DOLA.

AKITOA maoni yake mbele ya tume hiyo jana, Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), Jaji Mstaafu Damian Lubuva alisema kwamba muundo wa Muungano unapaswa kuangaliwa upya kikatiba, ili kuondoa malalamiko yaliyopo kwa muda mrefu.
Alisema suala la dola kwa nchi zilizoungana yaani Tanganyika na Zanzibar linapaswa kutambuliwa ili kila nchi iwe na mamlaka yake kamili.
“Kwa hali ilivyo sasa dola haiko Tanganyika wala Zanzibar, bali iko kwa Tanzania yote. Jambo hili linaleta manung’uniko mengi kwani Zanzibar kama ilivyo kwa Bara inahitaji kuwa na dola kamili.
Napendekeza mfumo wa Muungano ufuate matakwa ya wananchi kutoka kila upande, pia Katiba iainishe mambo ya Muungano ili kuondoa malalamiko kutoka kila upande,” alisema Jaji Lubuva.
Pia alisema Bunge linapaswa kuendelea na wajibu wake wa kutunga sheria na kuisimamia Serikali na siyo kufanya kazi za wizara.

Alisema kwa hali ilivyo sasa, Kamati za Bunge zimekuwa zikitoa maagizo na uamuzi kwa mambo mbalimbali kitu alichosema kuwa siyo sawa kwani hayo ni majukumu ya Serikali.
Jaji Lubuva alisema kitendo hicho kinaweza kudhoofisha utendaji wa Serikali, pia hakizingatii mgawanyo wa madaraka kwa mihimili ya dola.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here