MOTO WAITEKETEZA MTWARA, Nyumba ya Waziri wa TAMISEMI Hawa Ghasia yachomwa moto, Jengo la Mahakama laendelea kuteketea. - RAHA ZA PWANI

Habari za Hivi Punde

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Friday, January 25, 2013

MOTO WAITEKETEZA MTWARA, Nyumba ya Waziri wa TAMISEMI Hawa Ghasia yachomwa moto, Jengo la Mahakama laendelea kuteketea.

Picha hii si yatukio halisi la Mtwara na wala haina uhusiano na tukio hilo.

ASKARI wa kikosi cha kutuliza ghasia wametanda Mtwara na mabomu yanaendelea kupigwa tangu majira ya saa tano asubuhi. Nyumba kadhaa zimechomwa moto ikiwemo nyumba ya Waziri wa Tamisemi Hawa Ghasia pamoja na nyumba kadhaa zikiwemo za viongozi wa CCM.

Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Mtwara amesema hakuna aliyejeruhiwa lakini taarifa ya Mwandishi wa BBC Baruan Muhuza zinasema mwandishi wa habari mmoja wa mjini Mtwara amepigwa jiwe na kupasuka na kushonwa zaidi ya nyuzi nane kichwani.
Jengo la mahakama ya Mwanzo likiendelea kuteketea.

Chanzo cha tukio hilo kimeelezwa kuwa ni tuhuma za ushirikina kwa diwani mmoja ambae nyumbani kwake wameanguka watu wanaosadikiwa kuwa ni wachawi, kutokana na tukio hilo kuna baadhi ya watu wakitaka kutekeleza mambo yao ya kishirikina ndipo mkusanyiko huo ulipovamiwa na polisi.

Tukio hilo la vurugu zimekua zikiunganishwa na sakata la gesi kutokana na matamko yao ambayo wanasema hawataki gesi isafirishwe kwenda jijini Dar es Salaam. Mahakama ya Mwanza iliyopo karibu na Kituo Cha Mabasi nayonayo imechomwa  moto na inaendelea kuteketea muda huu.
Barabara za mji wa Mtwara zinawaka moto kutokana na vijana wengi walioandamana kuchoma moto matairi ya magari hali iliyosababisha mji mzima kutawaliwa na moshi mzito.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here