DAR YAGEUKA NYEKUNDU LEO!!! Wekundu wa Msimbazi watembeza kombe la Ubingwa wa Ligi Kuu mitaani. Walianzia Msimbazi, Magomeni, Ubungo, Buguruni hadi Dar Live Mbagala. Sherehe zinaendelea hapa Dar live. - RAHA ZA PWANI

Habari za Hivi Punde

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Sunday, May 27, 2012

DAR YAGEUKA NYEKUNDU LEO!!! Wekundu wa Msimbazi watembeza kombe la Ubingwa wa Ligi Kuu mitaani. Walianzia Msimbazi, Magomeni, Ubungo, Buguruni hadi Dar Live Mbagala. Sherehe zinaendelea hapa Dar live.

Shabiki wa Simba akifungua Shampain na kumwagia mashabiki wa timu hiyo mbele ya Jengo la Klabu hiyo.
 Mashabiki waliolewa Furaha wakiwashangilia baadhi ya wachezaji wa Simba waliokuwemo kwenye msafara huo.
 Hivi ndivyo mitaa ya Msimbazi ilivyoamka leo.
 Wengine walitoka vyumbani kuangalia mziki wa Simba, wakatoa hi!
 Wengine kando ya barabara wakicheza wimbo maarufu wa Young D, Dada Anaolewa.
 Hawa nao ni sehemu ya Shamra shamra hizo kila mtaa walipo pita Simba, hapa ni eneo la Faya, mashabiki waliotoka ndani wakiwapa big up simba.
 Yani kila Flate wakigombea kuchungulia japo waone 2.
 Mashabiki wa Shibam Magomeni 'Shibam' waliandaa mapokezi maalum ya kumuenzi mafisango nao wakawapokea hivi.
 Shibam waligusishwa kombe kiduchu iliwalibusu wakaligombea.

 Kipenzi cha mashabiki wa Simba Juma Kaseja akiliangalia Kombe nae baada ya kujiunga na msafara huo maeneo ya Usalama Magomeni Mapipa. Juma Kaseja Nyoso na baadhi ya wachezaji wengine walijiunga njiani kutokana na kuwepo kwenye kambi ya timu ya Taifa kujiandaa na michezo ya kimatifa.
 'Migomigo tunapitaaa..........mnatuona,' wakiimba mashabiki na wachezaji wa Simba.
 Hapa Mashabiki wa Mbagala wanapokea Msafara.
 Namna mashabiki wa Simba Mbagala walivyopokea Msafara huo.
 Jamani Simbaaaaaaaaaaa
 Waooooooooooo Karibuni Mbagalaaaaaaa

 Na sisi tumooooooooo!
 Baadhi ya Mashabiki wa Simba Mbagala walivyo lipokea kombe hilo na kulinadi.
 Wachezaji walitengewa eneo maalum!
 Alama hii ya vidole vitano ndiyo iliyoshamiri mitaani kote hadi ndani ya Dar Live, ikimaanisha ushindi wa goli tano walizomfunga Yanga wakati wa mchezo wao wa mwisho wa Ligi.
 Burudani kama kawa kila shabiki alijimwaga.
 Mashabiki waenzi zileeeee nao walikuja kuwakilisha wenzaoo!
 Nani Mshindi?
 Waenzi zile waliongezeka.

Walemavu nao wakapewa msaada wakuingia nda kulia ni Afisa habari wa Simba Ezekiel Kamwaga akisaidia kumbeba mlemavu huyo.
 Sisi ndo wanazi banaaaaaa!

Raha ya Ushindi nhiii basi tufurahi!

 Mwisho:

Na Philemon Solomon

SOMO la Tehama Katika shule za msingi  limeionekana kuwa ni somo linalopendwa na wanafunzi wa shule za msingi za serikali lakini wanakuwa hawalifurahii kutokana kutokuwa na Elimu hiyo kwa vitendo.

Changamoto hiyo inayozikumba karibu shule zote za msingi Nchini inajaribu kutatuliwa na Shirika lisilo la kiserikali lijulikanalo kama Fahamu Company lenye makao yake jijini Dar es  Salaam isipokuwa wanakosa ushirikiano kutoka kwa serikali.

Akizungumza na Waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Afisa utawala wa Shirika hilo Salmin Kisamo alisema kuwa, wameamua kufundisha somo hilo kwa shule zote za msingi ili kuwafungua wigo wa uelewa wa wanafunzi katika sayansi ya klutumia Kompyuta.

Kisamo aisema kuwa, katika uchunguzi mdogo walioufanya wamegundua kuwa waoto wengi wa shule za msingi hasa za serikali hawana uelewa katika somo la Tehama kwani wanakosa walimu wa kuwafundisha pamoja na vitendea kazi ikiwemo Kompyuta pamoja na simu.

Alisema, kwa kuanza kufundisha somo hilo tayari wameanza na shule mbili ambazo ni Mapinduzi pamoja na Gilman Rutihinda zote za Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

“Tumeanza na kufundisha shule mbili tu lakini tunampango wa kuendeleza mradi huu katika shule zote za msingi Nchini Tanzania hivyo tunaioma serikali iingize mkono wake  kusudi watoto wetu waende sambamba na tecknolojia ya kisasa ambayo ni Compyuta”, alisema Kisamo.

Alienderlea kusema kuwa, kwa sasa wanawachangisha wazazi wa watoto wenye mwitikio na mradi huo kiasi cha shilingi 3500 kwa mwezi ilki wapate pesa za kuwalipa walimu wanaofundisha somo hilo pamoja na kurekebishia vifaa wanavyotumia.

Hata hivyo Kisamo alkiserma kuwa ni wazazi wacheche tu ndio wenye mwtikio na wanao lipa fedha hizo kwani sio kila mzazi anauwezo wa kulipa fedha hizo.

Kisamo ameitaka serikali kusaidia kutatua changamoto waliyonayo ikiwemo uhaba wa Kompyuta ambapo kwa sasa wana kompyuta 36 tu za kufundishia wanafunzi zaidi ya 3000 pamoja na fedha za kuweza kuwalipa walimu wa kufundisha somo hilo kwani wazazi hawana uwezo wa kulipa 3500 kwa mwezi.

Nao wanafunzi wanaofundishwa masomo hayo wameiomba serikali iwasaidie katika kuongeza vifaa na pia wameonekana kulifurahia somo hilo.

Mwana funzi aliyejitambulisha kwa jina moja la Suzan alisema kuwa   anawaomba wazazi wawe na mwamko kwani nao eanataka kufanana na wanafunzi wa shule nyingine zisizo za serikali.

MWISHO

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here