MAANDAMANO MAKUBWA YAFANYIKA LIBYA LEO, NI YAKUDAI DEMOKRASIA NA KUPINGA SILAHA KUZAGAA MITAANI - RAHA ZA PWANI

Habari za Hivi Punde

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Saturday, September 22, 2012

MAANDAMANO MAKUBWA YAFANYIKA LIBYA LEO, NI YAKUDAI DEMOKRASIA NA KUPINGA SILAHA KUZAGAA MITAANI

Mmoja wa waandamanaji akipaza sauti leo mjini Benghazi kwenye mkutano uliofanyika baada ya maandamano.


Maelfu ya Walibya wamefanya mhadhara katika mji wa Benghazi, mashariki mwa Libya, kuunga mkono demokrasi na kuwapinga wapiganaji wa Kiislamu. Maandamano ya kupinga wapiganaji mjini Benghazi
Waandamanaji waliisihi serikali ya Libya iyapige marufuku makundi ya wapiganaji ambao wamekataa kukabidhi silaha zao tangu vita dhidi ya Kanali Gaddafi mwaka jana.

Waandamanaji wanataka serikali izidishe jeshi na polisi, na walimsifu balozi wa Marekani aliyeuliwa mjini humo juma lilopita. Waliimba wakati wakiandamana kuelekea medani kuu ya Benghazi.
Muandamanaji mmoja, Faisla al-Naas, alieleza sababu zao:

"Sisi tunaandamana kupinga kundi lenye silaha ambalo halidhibitiwi na serikali. Wapiganaji hawa wanafaa kujiunga na serikali ili watu wakae kwa salama. Nchi yetu imekuwa na mtafaruku."
Maandamano mengine ya kuunga mkono wapiganaji yalikuwa madogo sana.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here