Wakazi wa Kijiji hichowakimsikiliza Mkuu wa Wilaya Abdallah Ulega.
Diwani wa kata ya Pande Mikoma Abdallah Oga, akiwakaribisha wananchi kwenye mkutano huo ili waweze kumsikiliza Mkuu wa wilaya hiyo.
Baadhi ya wazee maarufu kijijini hapo wakifuatilia mkutano huo.
Said Powa Kilwa.
Baada ya Kaya 256 Wilayani Kilwa Mkoani Lindi kutia dosari kwenye mbalimbali zikiwemo za Tingi,
Kilwa Masoko, Kivinje na Njinjo wilayani humo kwa kukataa kuhesabiwa kwa madai ya kutokuwapo kipengele cha dini kwenye dodoso la sense Mkuu wa Wilaya hiyo Abdallah Ulega , anahaha vijijijini kuelimisha wananchi huku kwenye baadhi ya vijiji wanaohamasisha wenzao kupinga sense wakitiwa nguvuni.
Siku moja baada ya kutoa taarifa ya hali ya sense kwenye kikao cha Baraza la Maalum la Madiwani wa
Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa, Mkuu huyo alifanya ziara kwenye kijiji cha Pande kuzungumzana wananchi ili wajitokeze kwenye zoezi hilo ambalo likielekea ukingoni kabla ya kuongezwa muda wa siku 7.
Baada ya Kaya 256 Wilayani Kilwa Mkoani Lindi kutia dosari kwenye mbalimbali zikiwemo za Tingi,
Kilwa Masoko, Kivinje na Njinjo wilayani humo kwa kukataa kuhesabiwa kwa madai ya kutokuwapo kipengele cha dini kwenye dodoso la sense Mkuu wa Wilaya hiyo Abdallah Ulega , anahaha vijijijini kuelimisha wananchi huku kwenye baadhi ya vijiji wanaohamasisha wenzao kupinga sense wakitiwa nguvuni.
Siku moja baada ya kutoa taarifa ya hali ya sense kwenye kikao cha Baraza la Maalum la Madiwani wa
Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa, Mkuu huyo alifanya ziara kwenye kijiji cha Pande kuzungumzana wananchi ili wajitokeze kwenye zoezi hilo ambalo likielekea ukingoni kabla ya kuongezwa muda wa siku 7.
Hata hivyo wakazi wakijiji hicho walitoa masikitiko yao kwa
mkuu huyo wa wilaya kuwa pamoja na kuwalazimisha kwenda kuhesabiwa lakini
wanajisahau mno kwakutokwenda kutoa elimu kwa wananchi jambo ambalo
linasababisha sintofahamu kwa wananchi kutokana na kupata taarifa za upande
mmoja tu.
Wananchi hao ambao wapo kwenye makao makuu ya tarafa ya
Pande pia walihoji kitendo cha kuwanyima haki ya kukutana na tume inayoratibu
na kukusanya maoni ya katiba mpya badala yake tume hiyo imepelekwa kwenye kata
ambako hakuna uwezekano wa kufika wananchi wengi kutoa maoni yao.
No comments:
Post a Comment