Mrembo kutoka mkoa wa Pwani aibuka kidedea katika shindano la urembo la Kanda ya Mashariki 2012. - RAHA ZA PWANI

Habari za Hivi Punde

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Monday, September 3, 2012

Mrembo kutoka mkoa wa Pwani aibuka kidedea katika shindano la urembo la Kanda ya Mashariki 2012.

Chief Guest Miss Tanzania 2010 Genevieve Emmanuel akitoa zawadi kwa Salvina Kibona mshindi wa 4 Miss Eastern zone 2012
Top 3 winners Redds Miss Eastern zone 2012
TOP 5 MISS TALENT


Mshindi wa tatu wa shindano la urembo la mkoa wa Pwani Rose Lucas ameibuka mshindi wa kwanza katika kinyang’anyiro cha kumtafuta mrembo wa Kanda ya Mashariki kwa mwaka 2012.

Mrembo huyo ambaye hakuwa amepewa nafasi yoyote tangu mwanzo wa ushiriki wake, aliwashangaza mashabiki  na kushangiliwa mara kwa mara alipopanda jukwaani.
Rose Lucas ambaye ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha DSM mwaka wa kwanza  anasomea Shahada ya Biashara.

Washiriki wengine walioingia katika tatu 3 bora na ambao pia wataiwakilisha Kanda hiyo ya Mashariki katika Fainali za Mashindano ya urembo ya Redds Miss Tanzania ni, Irene Veda kutoka mkoa wa Lindi na Joyce Baluhi kutoka mkoa wa Morogoro.
 
Maajabu madogo yaliyotokea katika shindano hilo ni kwamba washiriki wale wale walioingia hatua ya Tano bora katika shindano dogo la vipaji Miss Talent, ndio hao hao walifanikiwa kuingia tena katika hatua ya Tano bora ya shindano hilo la kumtafuta mrembo wa Kanda ya Mashariki.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here